RAIS SAMIA ATOA NENO MIAKA 62 YA UHURU

RAIS SAMIA ATOA NENO MIAKA 62 YA UHURU

Size
Price:

Read more

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan

ameainisha changamoto zinazopaswa kupewa kipaumbele ikiwemo kufungamanisha

ukuaji wa uchumi na sekta za uzalishaji.

Rais Samia amesema hayo kwenye maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa

Tanzania Bara sanjari na Mkutano wa kwanza wa uzinduzi wa Dira ya Taifa ya

Maendeleo 2050, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete.

Aidha Rais Samia ametaka sekta mbalimbali za uzalishaji ziimarishwe zaidi ikiwemo

kilimo ambayo inakua kwa asilimia 4 tu kwa sasa tofauti na inavyotakiwa.

Pia amesisitiza kuimarishwa kwa ushiriki wa sekta binafsi ndani na nje ya nchi ili

kufanya wenyeji kuwa na utayari wa kupokea na kushirikiana na wageni wanaokuja

kuwekeza na kufanya biashara nchini.

Rais Samia amesema dira hiyo mpya itatakiwa kuzingatia kigezo cha kuongeza pato

la kila mwananchi kufikia dola za Kimarekani 3,000 kwa mwaka ambacho

hakikufikiwa katika dira ya mwaka 2000-2025.

Amesema kushindwa huko kulisababishwa na ukuaji wa uchumi kutojielekeza

kwenye sekta zinazogusa maisha ya watu wengi, hivyo umasikini vijijini haujapungua

kwa kasi iliyotarajiwa.

Kuhusu suala la Maadili ya Taifa (ethos), Rais Samia amesema ni muhimu taifa

kuwa na watu mahiri, makini na waadilifu ili kupata jamii inayochukia rushwa kila

mahali, inayojituma na kufanya kazi bila kusukumwa na inayopinga na kulaani

ukwepaji kodi.

Vile vile, Rais Samia ametoa wito kwa Watanzania wote ndani na nje ya nchi

(Diaspora) kushiriki kutoa maoni katika kuandaa Dira ya Taifa ya Maendeleo kupitia

njia za kisasa zitakazoainishwa na Tume ya Mipango.


Zuhura Yunus

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

0 Reviews

Contact form

Name

Email *

Message *