RAIS SAMIA AKABIDHI HUNDI YA BILIONI 2 KWA WAATHIRIKA WA MAAFA YA MAPOROMOKO YA ARDHI HANANG

RAIS SAMIA AKABIDHI HUNDI YA BILIONI 2 KWA WAATHIRIKA WA MAAFA YA MAPOROMOKO YA ARDHI HANANG

Size
Price:

Read more

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan

amekabidhiwa hundi yenye thamani ya shilingi Bilioni 2 kutoka kwa taasisi za umma

kwa ajili ya waathirika wa maafa ya maporomoko ya ardhi yaliyotokea wilayani

Hanang mkoani Manyara.

Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika Ikulu, Chamwino ambapo Rais Samia

amekabidhiwa hundi hiyo kutoka kwa Msajili wa Hazina, Bw. Nehemia Mchechu kwa

niaba ya taasisi mbalimbali za serikali.

Aidha, Rais Samia amesema lengo la kuwachangia waathirika hao ni kuweza

kuwapatia mahitaji muhimu ili waweze kurejea katika maisha yao ya kawaida.

Hali kadhalika, Rais Samia ameitaka Ofisi ya Waziri Mkuu kukamilisha tathmini ya

maafa hayo kwa waathirika ili serikali ianze mchakato wa kuwarejesha katika makazi

rasmi.

Rais Samia amewataka Watanzania kutunza mazingira kwa kusafisha na kuacha

kutupa takataka katika mitaro na kuhakikisha inazibuliwa kwa wakati ili mvua

zinaponyesha iweze kutiririsha maji.

Kwa upande mwingine, Rais Samia amezishukuru taasisi za umma,

wafanyabiashara na Watanzania kwa ujumla kwa kuonesha mshikamano katika

kusaidia waathirika wa maafa hayo.

Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Taasisi za Umma

wakiwemo Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, Waziri Mkuu Mhe.

Kassim Majaliwa pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na

Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama.

Zuhura Yunus

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

0 Reviews

Contact form

Name

Email *

Message *