Read more
Katika kukabilianana na kero wanazofanyiwa watalii katika fukwe mbali mbali,
Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa Wakaskazini Unguja imefanya operesheni
maalum na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa sabiini kwa makosa mbalimbali.
Akizungumza na Waandishi wahabari huko Ofisini kwake Mkototoni, Mkuu wa
Mkoa wa Kaskazini Unguja ambaae ni Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na
Usalama wa Mkoa huo Mheshimiwa RASHID HADID RASHID amesema
Operesheni hiyo ni maagizo ya Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi DK. HUSSEN ALI MWINYI ya kuwataka Wakuu wa Mikoa
kuweka Mazingira salama kwa wanachi na watalii katika maeneo yao.
Kwaupande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja, Kamishna
Msaidizi wa Polisi DANIEL SHILA ameeleza kuwa miongoni mwa waliokamatwa
katika Opersheni hiyo ni TWALIB SHAABAN AZUBERI (39) raia wa Kenya
ambae amekamatwa na dawa za kulevya.
Aidha amesema Jeshi la Polisi litaendelea kushirikiana na Vikosi vya Ulinzi na
Usalama katika Operesheni hizo ili kuhakikisha Mkoa huo unaendelea kuwa
Salama kwa wananchi na kuendelea kuvutia watalii.


0 Reviews