RAIS MWINYI AKUTANA NA WATURUKI

 


SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema imejikita kuleta mageuzi

makubwa kwenye sekta zote za maendeleo pamoja na kuwajengea uwezo

watu wake ili kuongeza kasi ya uchumi nchini.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi,

ameyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na Rais wa Taasisi ya Ufadhili

wa masomo nchini Uturuki (YTB) kutoka Wizara ya Utamaduni na Utalii

inayoshughulikia Mambo ya Nje, Bw. Abdullah Eren na ujumbe wake waliofika

kumtembelea.

Alisema, Serikali imepiga hatua kubwa kuimarisha miundombinu ya kisasa kwa

sekta zote za uchumi na jamii ikiwemo kuboresha ujenzi wa barabara, sekta za

elimu, afya na uwekezaji.

Dk. Mwinyi alisema, Uturuki imekua na ushirikiano wa katibu na Tanzania kupitia

ubalozi wake uliopo nchini kwa kuungamkono na kutekeleza miradi mbalimbali ya

Serikali ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara, ujenzi wa Uwanja wa

Amani na miradi mengine ya jamii, elimu, afya na ujenzi wa nyumba za maakazi

kwa wanchi wa Zanzibar kupitia kampuni ya “Orkun” kutoka Uturuki.

Aidha, ameishukuru Serikali ya Uturuki kwa ushirikiano wanaoutoa kwa Serikali za

SMT na SMZ hasa kuungamkono juhudi mbalimbali za maendeleo.

Rais, Dk. Mwinyi pia, aliipongeza Uturuki kwa kuendelea kuiunga mkono Tanzania

ikiwemo Zanzibar, hasa kutoa fursa nyingi za ufadhili wa masomo ya elimu ya juu

kwa fani mbalimbali ambapo Watanzania wengi wako nchini Uturuki wakiendelea

na mafunzo ya muda mfupi na mrefu.

Alisema, ufadhili ni moja ya msaada mkubwa unaotolewa na Serikali ya Uturuki

kwa Tanzania kwenye kukuza ushirikiano mwema uliopo baina ya mataifa mawili

hayo.

Pia, Dk. Mwinyi aliisifu Uturuki kwa kuwa na wawekezaji wengi Tanzania pamoja

na kampuni mbalimbali zinazoendendesha shughuli zao nchini.

Alisema kampuni hizo zimekua na ushirikiano mzuri na Seriikali za Tanzania

katika kuungamkono na kusaidia kwenye miradi ya maendeleo.

Naye, Bw. Abdullah Eren alimueleza Rais Dk. Mwinyi bado Serikali yao

inaendelea kutoa ufadhili wa masomo kwa Tanzania hususan, Zanzibar.

Amesema, Serikali ya Uturiki inatarajia kutoa ufadhili mkubwa wa masomo kwa

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Zanzibar kupitia vyuo vya amali vilivyopo

nchini na kumueleza Rais Dk. Mwinyi kwamba tayari wamefanya mazungumzo na

Waziri wa Elimu, Lela Muhamed Mussa kujadili suala hilo.


Bw. Aliwapongeza Wazanzibari kwa kuzikimbilia fursa nyingi zinazotolewa na

Serikali ya Uturuki na kueleza kuwa asilimia kubwa ya Wazanzibar wako Uturuki

kwa masomo na fursa nyengine za maendeleo.

Alisema, ujasiri wa Watanzania nchini Uturuki unatokana na ushirikiano na

uhisiano mzuri wa Dipolomasia uliopo baina ya pande mbili za ushirikiano.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Balozi wa Uturuki nchini Tanzanzia, Dk. Mehmet

Gulluoglu, alimuomba rais Dk. Mwinyi kuangalia uwezekano wa kuipatia fursa

Serikali ya Uturi kuanzisha makumbusho ya kidijitali itakayohusisha masuala ya

historia na utamaduni ili kuvutia zaidi watalii watakaoingia nchini.

Aidha, alieleza fursa hiyo pia itachochoa kasi ya ongezeko la watalii na fursa

nyingi za uwekezaji na biashara nchini.

BOSS TV

Hii ni Official blog ya BOSS MEDIA kwa habari za siasa, jamii, elimu, burudani na michezo tufuatilie kwa uhakika zaidi

Post a Comment

Previous Post Next Post