Waitara: Wanaoleta taharuki washughulikiwe

Waitara: Wanaoleta taharuki washughulikiwe

Size
Price:

Read more


MBUNGE wa Tarime Vijijini, Mwita Waitara, ameweka msimamo mkali Bungeni jijini Dodoma 

akiwataka viongozi wanaotoa matamko yanayozua taharuki na mifarakano kuondolewa kwenye 

nafasi zao mara moja, akisisitiza kuwa hawafai kuendelea kushika nyadhifa za uongozi.


Akichangia Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa mwaka 

2026/27, Waitara amesema haiwezekani baadhi ya watu “kutoboa mtumbwi” huku wengine wakikaa 

kimya bila kuchukua hatua za kinidhamu.


Amesema kauli na matendo ya viongozi yanapaswa kulinda umoja wa taifa badala ya kuchochea 

mgawanyiko au hofu miongoni mwa wananchi.


Aidha, amewataka Wabunge na viongozi wa ngazi mbalimbali kuheshimu wananchi na kuchunga 

maneno yao ili kuepuka kuibua taharuki isiyo ya lazima na kudumisha mshikamano wa kitaifa.


0 Reviews

Contact form

Name

Email *

Message *