RAIS DKT. MWINYI AMESHIRIKI CHAKULA CHA USIKU NA GPE IKULU  ZANZIBAR

RAIS DKT. MWINYI AMESHIRIKI CHAKULA CHA USIKU NA GPE IKULU ZANZIBAR

Size
Price:

Read more

 RAIS DK.MWINYI AMESHIRIKI CHAKULA CHA USIKU NA GPE IKULU

ZANZIBAR


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali

Mwinyi amejumuika pamoja na  Uongozi wa bodi ya Wakurugenzi wa

Shirika la Ushirikiano wa Elimu Duniani (GPE) ukiongozwa na Mwenyekiti

wake Dkt.Jakaya Kikwete, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania katika chakula cha usiku alichowaandaliwa  Ikulu Zanzibar tarehe

04 Disemba 2023.

Hafla hiyo pia imehudhuriwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa  GPE Laura

Frigenti pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali, Dini na Vyombo vya

ulinzi na usalama.

Aidha Vikao vya GPE vitafanyika Zanzibar na kufunguliwa kesho tarehe 05

hadi 06 Disemba ikiwa ni mara ya kwanza kwa shirika hilo la kimataifa

kufanya vikao vyake vya bodi barani Afrika.

Vilevile Shirika hilo limeisaidia Zanzibar katika sekta ya elimu fedha za

kigeni dola za kimarekani Milioni 11.7 kwa ajili ya kusaidia elimu ya msingi

ikiwemo miradi itakayoanza Januari 2024 kwa kujumuisha mafunzo ya

walimu, utendaji, usimamizi wa elimu , masuala ya jinsia na mjumuisho.

Kwa mujibu wa Dkt. Kikwete, ambaye ni Mwafrika wa kwanza kuongoza

GPE, shirika hilo hadi sasa limeishaipatia Tanzania jumla ya  Dola za

Kimarekani Milioni 332 (takriban shilingi 834,980,332,000.00) ili kusaidia

sekta ya elimu bara na Zanzibar.

0 Reviews

Contact form

Name

Email *

Message *