Hayo yamebainishwa Novemba 14, 2023 na Daktari kutoka Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Dodoma Dkt. Alemiana Alex ambapo amesema mambo ya kuzingatia katika kuepuka ugonjwa wa Kisukari ni pamoja na kuepuka kunywa pombe kupita kiasi, kupunguza matumizi ya sukari kwa wingi.
Unachotakiwa kufanya ni kula mbogamboga kwa wingi, kufanya mazoezi pamoja na kupunguza msongo wa mawazo na kuwa na desturi ya kupima afya mara kwa mara.