BAADA ya kipigo cha bao 5-1 kutoka kwa Yanga klabu ya Simba SC yenye maskani yake Msimbazi Dar Es Salaam, imeamua kuachana na kocha wake Robert Oliveira ‘Robertinho’ baada ya kukubaliana naye yaani makubaliano ya pande zote mbili.
Pia Simba imeachana na kocha wa viungo Corneille Hategekimana kwa makubaliano ya pande zote. Kwa sasa Simba ipo chini ya kocha wa makipa Daniel Cadena akisaidiwa na Suleiman Matola.

