Read more
GEITA: CHAMA cha Wachimbaji Wadogo Mkoa wa Geita (GEREMA) kimelalamikia uwepo wa changamoto ya kupanda kwa kemikali ya Sianidi inayotumika maalum kwa shughuli za uchechuaji wa madini ya dhahabu
Katibu wa GEREMA, Misana Nyabange amesema bei ya kemikali ya sianidi kutoka laki tano hadi milioni moja.
Waziri wa Madini, Anthony Mavunde amesema serikali itafanya kikao maalum cha tathimini kesho Desemba 2, 2025 ili kujadili kupanda kwa tatizo hilo.
Waziri wa Madini, Anthony Mavunde ametoa kauli hiyo akiwa wilayani Nyang’hwale mkoani Geita katika hafla ya ugawaji wa leseni kwa wachimbaji wadogo iliyofanyika Kijiji cha Nyijundu.
Katika kikao hicho wataalamu kutoka Tume ya Taifa ya Madini pamoja na
Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali watakuwepo.
Matumizi ya kemikali ya sianidi ni teknolojia za kisasa za uchenjuaji madini
ya dhahabu yenye ufanisi wa kati ya asilimia 90-98 tofauti na asilimia 40-48 ya
madini ya zebaki.




0 Reviews